Jinsi ya Kutumia Programu ya IDM Bure Kwa Miaka 10

IDM IDM

Progamu za kupakua au kudownload zimekua nyingi sana siku hizi lakini watu wengi kwa sasa wanatumia programu ya IDM au Internet Download Manager kushusha vitu mbalimbali kwa kutumia Kompyuta zao, lakini tatizo la programu hii ni kwamba unaweza kuitumia bure kwa muda wa siku 30 yani mwezi mmoja baada ya hapo inakubidi ufanye malipo ili uweze kuendelea kutumia.

https://www.youtube.com/watch?v=YvZHv43bjIk

Kwa sababu mbalimbali inawezekana umeshindwa kulipia programu hii lakini unauhitaji mkubwa sana na programu hii kwani kiukweli programu hii ni msaada mkubwa sana hasa pale unapotaka kupakua vitu kutoka mitandaoni bila kupoteza muda mwingi. Ifuatayo ni namna ya kutumia programu hii bure kabisa bila kulipia kiasi chochote cha muhimu ni kufuata hatua hizi kwa umakini.

Advertisement

Basi moja kwa moja twende tukaanze somo letu, ili kuanza unatakiwa kuwa na internet kwenye kompyuta yako na pia hakikisha una bando kiwango cha chini kiwe MB50, ukiwa na hayo yote moja kwa moja bofya kwenye kitufe hapo chini kisha pakua programu hiyo iliyoko kwenye mfumo wa ZIP.

Internet Download Manager 8.12 MB

Baada ya hapo fungua file lako kwa kutumia programu maalumu ya Zip ambayo iko moja kwa moja kwenye kompyuta yako, kisha fungua folder lako na anza kufanya instalation ya programu ya IDM ambayo imeandikwa “idman625build16.exe” baada ya kuifadhi au kuinstall programu yako hakikisha haubonyezi kitufe cha FINISH bali ingia kwenye folder lilioandikwa “Crack” kisha utakuta ndani kuna programu iliyo andikwa “IDM Man“, Copy programu hiyo na paste kwenye sehemu yalipo mafaili ya IDM. Moja kwa moja nenda kwenye progarmu yako ya IDM na bofya “Finish” baada ya hapo nenda kwenye programu iliyoandikwa KEY kisha bofya mara mbili na bofya OK, kwa kufanya hivyo utaweza kutumia application ya IDM kwa miaka 10 bure ukiwa na uwezo wa ku-update.

Kwa kujifunza kwa umakini zaidi angalia video hiyo hapo juu ambayo itakusaidia kujifunza hatua, pia kama unayo maoni ushauri au kama umekwama mahali popote comment na tutakusaidia au unaweza kutembela page ya facebook ya Tanzania Tech na ukauliza swali lako na tutakusaidia.

2 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use