in

Jifunze Hapa Jinsi ya Kuchaji Simu Yako kwa Kutumia Limao

Jifunze hatua kwa hatua jinsi ya kutengeneza battery kwa kutumia limao

Jifunze Hapa Jinsi ya Kuchaji Simu Yako kwa Kutumia Limao2:39

Habari karibu kwenye maujanja, leo nina kuletea njia ambayo kwa namna moja ama nyingine lazima utakuwa unaijua au umeshawahi sikia. Sababu za kuileta hapa ni kuwa watu wengi wamekuwa wakiuliza kupitia mitandao yetu mbalimbali ya kijamii na hivyo inabidi leo nikuletee hapa hatua kwa hatua.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Mahitaji

Kumbuka njia hii ni rahisi na mtu yoyote anaweza kufanya lakini kitu cha muhimu ni kuwa na mambo yafuatayo,

  • Unatakiwa kuwa na limao ambalo limeiva vizuri au lenye maji ya kutosha.
  • Unatakiwa kuwa vitu vigumu vya copper kama pini za kuwekea makaratasi kwenye notes Board.
  • Unatakiwa kuwa na misumari.
  • Unatakiwa kuwa na Waya.

Njia za Kufuata

Unatakiwa kuchukua limao na kulisugua kwa upande juu ya meza lakini usisugue limao hilo kwa nguvu, njia hii ni muhimu kwa sababu inafanya limao lijae maji ya kutosha ambayo ni muhimu kwenye hatua hizi za kutengeneza battery ya kuchaji simu yako.

Baada ya hapo chukua copper na chomeka upande mmoja wa limao na chukua misumari chomeka upande wa pili wa limao, chukua waya na zungushia kama inavyo onekana kwenye video hapo juu.

Baada ya hapo unganisha waya upande mmoja wa misumari, hakikisha waya mmoja unaenda upande wa kushoto na waya mwingine unaenda upande wa kulia. Baada ya hapo utakuwa umekamilisha kuweza kutengeneza batter ambayo inaweza kuchaji simu yako. Kumbuka fanya njia hizi kwa usahihi kwani hatuta husika na uharibufu wowote utakao tokea.

Kutumia App ya WhatsApp kwa Lugha ya Kiswahili

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

2 Comments