Huawei P9 Kuzinduliwa South Africa

Huawei P9 Huawei P9

Siku zilizopita tuliona Huawei ikizindua simu yake bomba ya Huawei p9, kwa mojibu wa huawei simu hii ni moja kati ya simu ambazo zinatumia teknolojia mpya ya Leica ikiwa inakupa uwezo wa kutumia kamera mbili zilizopo nyuma ya simu hiyo bomba ya Huawei.

Kama wewe ni mmoja kati ya wale watu wanaopenda picha pamoja na selfie simu hii ni bomba sana kwaajili yako, pia simu hiyo inaonekna kuwa na kioo chenye uwezo mkubwa sana wa kuonyesha video ya 1080p vilevile simu hii ina kuja na processor mpya ya Kirin 955 2.5GHz 64-bit ARM-based processor ikiwa inasaidiwa na ram ya 2GB, ikiwa na uwezo wa kukaa na chaji kwa kiwango cha aina yake kwani battery ya huawei P9 ina kiwango cha  3000mAh ambapo inasemekana ni moja kati ya simu za kampuni hiyo inayokaa na chaji zaidi kuliko zingine.

Simu hii itakuwa ikiuzwa kwenye maduka yote ya simu ya mitandao ya simu ya huko nchini south africa kuhusu bei inasemekana simu hiyo itauzwa kati ya randi za south africa R11 999  mpaka R13 499 kwa huawei P9 plus. Simu zote hizi zinasemekana nakuja na vifurushi mbalimbali kama mtu atanunua lakini hii ni kwa south africa tu..

Advertisement

Kama umeipenda hii usisite kulike page yetu ya Facebook pamoja na Twitter ili kupata habari mpya pindi zinapotoka, pia kwa kujifunza mambo mbalimbali kwa vitendo unaweza ku subscribe kwenye Youtube Channel yetu hapa Tanzania tech blog.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use