in

Instagram Yatangaza Kusitisha App Yake ya Kuchati ya Direct

Sasa instagrama yarudisha sehemu ya kuchat kwenye app ya Instagram

Instagram Yatangaza Kusitisha App Yake ya Kuchati ya Direct

Inawezekana kwa namna moja ama nyingine hii ni mara yako ya kwanza kusikia app ya kuchati kutoka instagram inayoitwa direct, hii inatokana na kuwa app hii kwa namna moja ama nyingine ilikuwa haipatikani hapa Tanzania.

Lakini kama wewe ni msomaji wa Tanzania Tech, najua umeshawahi kujaribu app hii kwani kipindi cha nyuma tulishawahi kuonyesha jinsi ya kudownload app hiyo na kuinstall kwenye simu yako ya Android.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
App ya Instagram Direct
Muonekano wa App ya Direct Kutoka Instagram

Sasa kama hukuweza kujaribu app hiyo kipindi hicho, ripoti mpya kutoka Instagram zinasema kuwa app hiyo imetangazwa kusitishwa na haitokuwa inaboreshwa tena na Instagram. Kwa mujibu wa ripoti kutoka tovuti ya TechCrunch, instagram imesema inasitisha app hiyo na matumizi yote ya app hiyo yatarudisha kwenye sehemu ya DM ndani ya App ya Instagram.

Kama ulikuwa huijui app ya Direct, app hiyo ilikuwa inakupa urahisi wa kuchati na ndugu na jamaa ambao wapo kwenye mtandao wa Instagram huku pia ikikupa urahisi wa kuangalia Srories kutoka kwenye akaunti mbalimbali za watu ulio wafuata.

Kwa sasa Facebook ipo kwenye mpango wa kuunganisha programu zake za Facebook, Instagram na WhatsApp ili kutoa urahisi kwa watumiaji kutumia programu hizo kwa urahisi pamoja na wafanya biashara kuweza kutangaza biashara zao kwa mapana zaidi.

Instagram Yatangaza Kusitisha App Yake ya Kuchati ya Direct
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.