in

Samsung Yazindua Space Monitor Kioo Kipya cha Kompyuta

Kioo kipya cha Samsung chenye kuchukua nafasi ndogo ya meza yako

Samsung Yazindua Space Monitor Kioo Kipya cha Kompyuta

Wakati tukikaribia kwenye mkutano wa CES 2019, Kampuni ya Samsung imeanza mapema kwa kutangaza ujio wa kioo kipya cha kisasa kwaajili ya kompyuta. Kioo hicho kinachoitwa Samsung Space Monitor, kimetengenezwa maalum kwaajili ya kutoshea kwenye meza ndogo au kwa mtu ambaye anapenda kupata nafasi kubwa ya meza pale anapokuwa hatumii kompyuta.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Samsung Space Monitor imetengenezwa na mkono maalum ambao huu ufungwa kwenye meza na pale unapotaka kutumia kioo hicho unaweza kuvuta kioo hicho kwa mbele na mkono huo hujikunja ili kioo hicho kiweze ku-kufikia. Vilevile mkono huo ambao pia huficha nyaya ambazo mara nyingi uchukua nafasi kubwa pale mtu anapokuwa anatumia kioo cha kompyuta.

Samsung-2019-Monitors_main_1-min

Samsung Space Monitor inakuja kwa size mbili tofauti, kioo cha inch 27 chenye QHD resolution na kioo cha inch 34 chenye teknolojia ya 4K UHD. Kioo hicho pia kinakuja na sehemu ya HDMI pamoja na viunganishi vya USB pamoja na power cable.

Samsung Yazindua Space Monitor Kioo Kipya cha Kompyuta

Kwa sasa bado Samsung haijatangaza bei ya kioo hicho, kujua zaidi kuhusu kioo hichi endelea kutembelea Tanzania Tech tutakuwa mubashara kwenye mkutano wa CES 2019.

Samsung Yazindua Space Monitor Kioo Kipya cha Kompyuta
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.