in

Uchunguzi Waanza kwa Wanaotuma Meseji za Kitapeli

Wanaotuma meseji za kitapeli Tanzania sasa kubainika

meseji za kitapeli

Ripoti kutoka kwenye tovuti ya Mwananchi zinasema kuwa, Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kupitia kitengo cha upelelezi wa makosa ya mtandaoni, (Cybercrime investigation unit) kinafanya uchunguzi kuwabaini wanaotuma ujumbe mfupi wa simu za mkononi kwa nia ya kuwatapeli wananchi.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Barnabas Mwakalukwa, leo Juni 6, imesema yeyote aliyetapeliwa anatakiwa kutoa taarifa kwani jumbe hizo zina lengo la kuwatapeli na kuwaibia fedha wananchi.

“Tunawataka wananchi kuacha kutumia simu na mitandao ya kijamii vibaya na badala yake itumike kuhabarisha na kuelimisha jamii juu ya mambo mbalimbali ya maendeleo,” imesema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imesema, baadhi ya jumbe hizo ni zile zinazosema. ‘Ile hela tuma kwa namba hii’ au ‘usipige kwa sasa, spika imeharibika, tuma ujumbe,’ au ‘Mjukuu wangu ile ndagu niliyokutumia imefanya kazi na sasa unapata wateja wengi… sasa njoo uchukue ndagu nyingine ya mvuto.’

Taarifa kutoka tovuti ya Mwananchi.

Tovuti za Kujifunza Kutengeneza Apps na Website Bure 100%

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.

2 Comments