Rihanna Aituhumu Snapchat kwa Sababu ya Tangazo Lao

Amesema kuwa Snapchat sio mtandao anao upenda zaidi
Rihanna Aituhumu Snapchat kwa Sababu ya Tangazo Lao Rihanna Aituhumu Snapchat kwa Sababu ya Tangazo Lao

Weekend hii sakata jipya limeibuka mtandaoni baina ya mwanamzuiki maarufu kutoka marekani Rihanna, pamoja na mtandao maarufu wa Snapchat. Sakata hilo limekuja baada ya Snapchat kuruhusu kuweka tangazo la mchezo au Game, ambapo tangazo hilo liliwataka watumiaji wa mtandao kuchagua jibu moja kwenye picha kupitia game hiyo.

Tangazo hilo ambalo linatolewa na game maarufu ya Would You Rather, lilimuweka mwanamuziki Rihanna pamoja na mwanamuziki mwingine Chris Brown ambao walishawahi kuwa wapenzi. Sasa tatizo halipo kwenye picha hizo kuwekwa pamoja, bali kwenye picha hizo unatakiwa uchague chaguo moja gumu huku maneno yakiwa yameandikwa “utachagua umpige nani kati ya wawili hao kwenye picha hiyo” ikiwa ni lazima uchague mmoja kati ya wawili hao.

Sasa kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rihanna aliwatuhumu snapchat kwa kuruhusu picha hiyo isiyo na maadili huku ikiituhumu Snapchat kuwa inasisitiza unyanyasaji wa kijinsia kwa kuruhusu Tangazo hilo. Rihanna alisema kuwa hata hivyo Snapchat sio mtandao anao upenda zaidi huku akiita kitendo hicho cha kuruhusu tangazo hilo ni kitendo cha kijinga.

Advertisement

Snapchat kupitia mitandao mbalimbali ilitangaza kuomba msamaa juu ya kuruhusu tangazo hilo na kusema kuwa, tangazo hilo liliruhusiwa kwa bahati mbaya na kusema kuwa imeondoa tangazo hilo na inafuatilia kwa undani zaidi ili kujua jinsi tukio hilo lilivyo tokea na kuhakikisha kuzuia isitokee tena kwa siku za mbeleni.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use