in

Je Hii Ndio Tarehe ya Kutoka kwa Bidhaa Mpya za Apple?

Bidhaa za Apple

Msimu wa spring unakaribia uko marekani, huu ni wakati maalumu kwa kampuni ya simu za mkoni Apple kutoa matoleo mapya ya bidhaa zake kama iPhone, iPad na watch band, hayo yamedhibitishwa na blog ya marekani  iitwayo 9to5 Mac.

Tarehe 15 March siku ya jumanne mwaka 2016 ni tarehe maalumu kwa kampuni hiyo ya Apple kwani, ndio siku kampuni hiyo itakua ikizindua bidhaa zake mpya za iPhone, iPad na watch band taarifa zinaendelea kusema kutoka blog ya 9to5 Mac.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Hata hivyo blog hiyo inaendelea kusema kua Apple itatoa bidhaa zake mpya kama vile 4– inch iPhone 5SE na iPad Air 3.

Simu zote mpya zita jumuisha uongezaji wa ubora wa kamera na kuongezwa kwa application kadhaa katika vifaa hivyo, hata hivyo blog hiyo maarufu marekani inasema kuwa iPad Air 3 itakuwa na kamera nzuri ya nyuma itakayokua na ubora zaidi kuliko matoleo yake ya nyuma ya iPad. Na pia kwa upande wa watch band Apple itaongeza rangi nyingi mbalimbali pamoja na kuweka mikanda ya plastic kwenye saa hizo maharufu kama watch band. Kampuni ya Apple haikutoa maoni yoyote kuhusiana na taarifa hizi.

Je Hii Ndio Tarehe ya Kutoka kwa Bidhaa Mpya za Apple?
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Zifahamu Hizi Hapa Bei za Simu Mpya za Redmi Note 13

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.