Popular Now
Claude Mythos Toleo Jipya la AI Lenye Kutishia Usalama 5

Claude Mythos Toleo Jipya la AI Lenye Kutishia Usalama

Google is Introducing a Search Bar Within Play Store Reviews 6

Google is Introducing a Search Bar Within Play Store Reviews

Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026 7

Samsung Will Discontinue its Messages app in July 2026

Watumiaji wa WhatsApp

Programu ya WhatsApp Yafikisha Watumiaji Bilioni 1.5 kwa Mwezi

Facebook kupitia mkurugenzi wake Mark Zuckerberg, ilitangaza kununua programu ya WhatsApp hapo mwaka 2014 kwa dollar za kimarekani billion $19.

Miaka minne badae thamani ya mtandao huo imepanda na watumiji wake kuongezeka kwa kasi zaidi. Ukilinganisha wakati programu hiyo ina nunualiwa na facebook whatsapp ilikuwa na idadi ya watumiaji zaidi ya milioni 450 lakini hivi leo idadi ya watumiaji wa mtandao huo imeongezeka na kufikia bilioni 1.5

Vile vile mtandao huo wa WhatsApp umeongezeka idadi ya watu wanaotuma meseji hadi kufikia idadi ya meseji zaidi ya bilioni 60 kwa siku moja. Hii ni tofauti kubwa kutoka mwezi wa saba mwaka jana 2017 wakati mtandao huo ulipokuwa na watumiaji bilioni 1.3 kwa mwezi pamoja na watumiaji zaidi ya bilioni 1 kila siku.

Mbali na hayo Mark Zuckerberg, amebainisha kuwa kwa sasa mtandao WhatsApp pamoja na instagram ni mitandao inayo ongoza kwa watumiaji wengi wa sehemu ya Stories ukilinganisha na programu nyingine kama snapchat. WhatsApp na instagram zote zina watumiaji wa stories zaidi ya milioni 300 kila siku kulinganisha na mtandao wa Snapchat ambao unao watumiaji wa Stories milioni 178 kwa siku.

Haya ni mafanikio makubwa sana ya mtandao wa WhatsApp ni wazi kuwa uamuzi wa facebook kununua WhatsApp kwa dollar bilioni $19 ulikuwa ni uamuzi mzuri sana japo kwa kipindi hicho ilikua inaonekana kuwa facebook imelipa pesa nyingi sana. Ni wazi kuwa facebook itanza kurudisha faida yake kwa kutengeneza pesa nyingi zaidi tena ukizangati sasa inayo programu mpya ya WhatsApp ya Biashara.

Previous Post
WhatsApp ya Biashara

Hatimae WhatsApp ya Biashara Sasa Yafika Rasmi Tanzania

Next Post
telegram-x

Telegram Yaja na App Mpya ya Android ya Telegram X