in

Seezi: Tovuti ya Kuuza na Kununua Bidhaa Bila Udanganyifu

Seezi imekuja na mpango mzuri wa kumaliza tatizo la utapeli kabisa.

Seezi: Tovuti ya Kuuza na Kununua Bidhaa Bila Udanganyifu

Kama unavyojua, soko la mtandaoni limekuwa likikua kwa kasi sana katika miaka ya hivi karibuni. Hata hivyo, pamoja na maendeleo haya ya kiteknolojia, tatizo la udanganyifu wa mtandaoni limekuwa likiongezeka kadiri siku zinavyozidi kwenda.

Kwa sababu hiyo, tovuti ya Seezi imekuja na mpango mzuri wa kumaliza tatizo hili kabisa.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Katika makala hii, tutakuonyesha jinsi Seezi inavyofanya kazi kuhakikisha kuwa unanunua bidhaa kwa usalama zaidi na kuaminika.

Seezi: Tovuti ya Kuuza na Kununua Bidhaa Bila Udanganyifu

Hatua ya kwanza: Kuwa na uhakika na muuzaji

Kabla ya kununua bidhaa yoyote kwenye tovuti ya Seezi ni vyema kufahamu kuwa kabla ya muuzaji kuweka bidhaa zake kwenye tovuti ya Seezi ni lazima muuzaji huyo ahakikiwe na timu ya seezi na ajulikane duka lake mahali lilipo. Hii itakusaidia kuepuka kudanganywa na wadanganyifu ambao hutoa bidhaa kwenye mitandao ya kijamii na kisha kutoweka kabla ya kutoa bidhaa.

Hatua ya pili: Muuzaji lazima awe na kitambulisho cha kitaifa

Kitambulisho cha kitaifa au namba ya NIDA ni muhimu sana. Ni hatua ya ziada seezi ya kuhakikisha kuwa muuzaji ni halali na kwamba unanunua kutoka kwa muuzaji halali. Hii itakusaidia kuepuka wadanganyifu wanaojifanya kuwa ni wafanyabiashara halali na kuondoka na pesa yako.

Hatua ya tatu: Uhakiki wa Simu

Kuhakikisha kwamba simu unayotumia inathibitishwa na namba yako ya NIDA ni hatua nyingine ya kuhakikisha kuwa unanunua bidhaa kutoka kwa muuzaji halali. Hii inasaidia kuepuka wadanganyifu ambao hujifanya kuwa wauzaji halali kwa kutumia simu za wengine.

Hatua ya nne: Usajili wa kimwili

Usajili wa kimwili unafanywa mahali ambapo duka la muuzaji liko. Hii inasaidia kuthibitisha kuwa muuzaji ni halali na kwamba wanauza bidhaa zao kutoka mahali halali. Kwa njia hii, unaweza kuepuka wadanganyifu ambao hujifanya kuwa wauzaji halali lakini wanapokea malipo yako na kutoweka kabisa.

Hatua ya tano: Muuzaji anasaini fomu maalum

Hatua hii ni ya mwisho katika kuhakikisha kuwa unanunua bidhaa kutoka kwa muuzaji halali. Muuzaji anasaini fomu maalum kuthibitisha uhalali wake na kwamba yeye ni mmiliki halali wa biashara.

Seezi: Tovuti ya Kuuza na Kununua Bidhaa Bila Udanganyifu

Kwa hivyo, hii inahakikisha kuwa unanunua kutoka kwa muuzaji halali na unaweza kuwa na uhakika kwamba bidhaa unazonunua ni halali na za ubora wa juu.

Kwa ufupi, Seezi ni tovuti bora ya kuuza na kununua bidhaa. Kwa mujibu wa Ramadhan Kilindo “Tunaahidi kutoa huduma bora zaidi kwa wateja wetu na kuhakikisha kuwa unanunua bidhaa kutoka kwa muuzaji halali”.

Tembelea Tovuti ya Seezi Hapa

“Kupitia hatua zilizotajwa hapo juu, tunaweza kuhakikisha kuwa unanunua bidhaa kwa usalama na uhakika. Kama Mtanzania, tunajukumu la kulinda na kujenga jamii yetu, na kupitia Seezi, tunataka kufanikisha hilo na kujenga uaminifu kati yetu na wateja wetu”.

Seezi
Price: Free

Kwa sasa unaweza kutembelea tovuti ya Seezi na kufurahia huduma bora ya kuuza na kununua bidhaa, kupitia seezi.co.tz pia unaweza kupata app ya Android kupitia Play Store.

Seezi: Tovuti ya Kuuza na Kununua Bidhaa Bila Udanganyifu
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Ifahamu Simu Sahihi Kwa Content Creators

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.