Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Fahamu simu gani ya kununua kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s
Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Hivi karibuni kampuni ya Infinix imeingiza sokoni simu mpya ya Infinix Zero X Pro simu ambayo tumeisikia sana kwenye habari mbalimbali, kwa upande mwingine kampuni ya Vivo nayo pia siku za nyuma ilizindua simu yake mpya ya Vivo Y53s.

Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Kupitia makala hii tutaenda kuangalia tofauti kubwa za simu hizi mbili kwa upande wa sifa, muonekano na mengine ya muhimu. Na tumaini kuwa hadi mwisho wa makala hii utaweza kujua ni simu gani ambayo ni bora kwako.

Advertisement

Muonekano

Ni kweli kuwa Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s zote zina kuja na muonekano mzuri lakini ni wazi kuwa Infinix Zero X Pro inakuja na muonekano bora na wa tofauti sana.

Hii ni kutokana na muonekano wake wa nyuma ambao haupatikana kwenye simu nyingi za sasa.

Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Ni wazi kuwa kwa upande wa muonekano Infinix Zero X Pro ina muonekano wa tofauti kuliko Vivo Y53s. Hii ni kutokana na muonekano wa Vivo Y53s kutumika kwenye simu nyingi sana.

Kioo

Infinix Zero X Pro inakuja na kioo cha inch 6.67, wakati Vivo Y53s inajua na kioo cha inch 6.58. Wakati infinix Zero X Pro ikiwa na kioo kikubwa kwa upande wa size ya kioo, lakini pia Infinix Zero X Pro inakuja na kioo bora cha AMOLED chenye kuonyesha rangi vizuri zaidi tofauti na kioo cha IPS LCD ambacho kina tumika kwenye simu ya Vivo Y53s.

Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Kwa upande wa kioo ni wazi kuwa Infinix Zero X Pro ni bora zaidi kwani kioo cha AMOLED ni bora sana kuliko kioo cha IPS LCD hasa kwenye upande wa rangi.

Mbali na hayo kioo cha infinix Zero X Pro kina resolution ya 1080 x 2400, wakati Vivo Y53s ina 1080 x 2408.

Tofauti nyingine kubwa ambayo inapatikana kwenye simu ya Infinix Zero X Pro ni pamoja na kuwa kioo cha simu hii kina kuja na 120Hz Refresh rate wakati Vivo Y53s haina teknolojia hii kwenye kioo chake.

Kamera

Kwa upande wa kamera hapa ni wazi kuwa Infinix Zero X Pro imeshinda kwa kuwa simu hii inakuja na teknolojia ambayo haipo kabisa kwenye simu ya Vivo Y53s.

Mbali ya kuwa kamera za Infinix Zero X Pro ni kubwa zaidi lakini pia kamera hizi zina uwezo mkubwa zaidi.

Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Kama unataka kupiga picha za tofauti ambazo pia utaweza kuzoom vitu kwa ukaribu zaidi basi kamera hizi tatu (Megapixel 108, MP 8, MP 8) za Infinix Zero X Pro ni bora zaidi kwako. Hii ni kutokana na kamera hizi kuwa na uwezo wa 60x Periscope Lens ambayo inaweza kuzoom vitu kwa ukaribu zaidi, ikiwa pamoja na uwezo wa kupiga picha Mwezi na kufanya uonekane karibu zaidi.

Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Kwa upande wa Vivo Y53s unapata kamera tatu pia ambazo zinakuja na Megapixel 64 na nyingine mbili ambazo zina Megapixel 2 kila moja.

Mbali na hayo kamera za Infinix Zero X Pro kwa pamoja zinaweza kuchukua video za 4K, wakati kamera za Vivo Y53s zinaweza kuchukua video za hadi 1080p pekee.

Pia tofauti nyingine ni kuwa Zero X Pro inakuja na flash ya Dual-LED flash kwa mbele, wakati Vivo Y53s haina flash kwa mbele.

Sifa za Ndani

Kwa upande wa sifa ni wazi kuwa Infinix Zero X Pro inashika namba moja hii ni kutoka na kuwa simu hii inatumia processor yenye chipset ya Mediatek Helio G95, wakati Vivo Y53s inatumia chipset ya Mediatek Helio G80 ambayo ni ndogo.

Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Mbali na hayo Infinix Zero X Pro inakuja na CPU yenye speed zaidi ya Octa-core (2×2.05 GHz Cortex-A76 & 6×2.0 GHz Cortex-A55), wakati Vivo Y53s inakuja na CPU yenye Octa-core (2×2.0 GHz Cortex-A75 & 6×1.8 GHz Cortex-A55).

Ni wazi kama wewe ni mpenzi wa game basi simu ya Infinix Zero X Pro itakufaa zaidi kutokana na kuwa na chipset bora zaidi kwa game, bila kusahau CPU yake pia inakuja na speed zaidi kuliko Vivo Y53s.

Battery

Kwa upande wa battery Vivo Y53s inakuja na battery kubwa ya 5000 mAh, wakati Infinix Zero X Pro inakuja na battery ya 4500 mAh. Mbali ya hayo simu ya Infinix Zero X Pro inakuja na teknolojia bora ya Fast charging ya hadi 45W ambayo kwa mujibu wa Infinix inaweza kujaza simu yako hadi asilimia 40 ndani ya dakika 15 pekee.

Hizi Hapa Tofauti kati ya Infinix Zero X Pro na Vivo Y53s

Hitimisho

Ni wazi kuwa simu ya Infinix Zero X Pro ni simu bora kuliko Vivo Y53s, hii ni kutokana na kuwa na muonekano bora na watofauti, kioo bora zaidi cha AMOLED, kamera kubwa ya Megapixel 108 yenye uwezo wa kuchukua picha za bora, pamoja na processor bora ya Mediatek Helio G95, bila kusahau uwezo mzuri wa kujaa chaji kwa haraka kutokana na teknolojia ya Fast charging.

Kwa maoni yangu binafsi, Vivo Y53s na Infinix Zero X Pro ni simu ambazo zote zinauzwa bei zinazo fanana, hivyo kama unahitaji sifa zaidi na uwezo zaidi basi Infinix Zero X Pro ni simu bora zaidi.

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use