in

Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa

Akaunti hacked ni Barack Obama, Joe Biden, Elon Musk, Bill Gates, Kanye West na nyingine

Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa

Habari mpya hivi leo zinasema kuwa, mtandao wa Twitter umedukuliwa na akaunti za kampuni kubwa na watu maarufu kutumika kufanya utapeli.

Kwa mujibu wa mtandao huo, akaunti za kampuni hizo na watu maarufu ni pamoja na Raisi mstaafu wa marekani Barack Obama, Joe Biden, Elon Musk, Bill Gates, Kanye West, Michael Bloomberg, pamoja na akaunti ya kampuni ya Apple.

Install Android App
Price: Free
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot
  • Nyimbo Mpya Screenshot

Twitter imethibitisha kuwa ilichukua hatua kali ya kuzuia tweets mpya kutoka kwa kila mtumiaji aliyethibitishwa (Verified), ikiwa pamoja na kufunga akaunti zote zilizozudukuliwa.

Hata hivyo, Twitter ilitangaza kuwa haito rudisha akaunti hizo kwa watumiaji wake mpaka pale itakapo hakikisha kuwa akaunti hizo ziko salama kwa asilimia 100.

Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa

Hata hivyo inasemekana kuwa baadhi ya miundo mbinu ya ndani ya kampuni ya Twitter ilitumika kutekeleza udukuaji huo, ndio maana inasemekana kuwa akaunti za watu maarufu ambazo pia zilikuwa na ulinzi wa ziada (two-factor authentication) nazo pia ziliweza kudukuliwa.

Kwa sasa inasemekana baadhi ya akaunti tayari zimeanza kuruhusiwa kutweet, huku Twitter ikiendelea kufuatilia na kuongeza ulinzi wa akaunti hizo.

Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa

Inasemekana Akaunti ya kwanza kudukuliwa ilikuwa ni akaunti ya CEO wa kampuni ya Tesla, ambapo wadukuaji walikua wakifanya utapeli kwa kutumia mtandao wa Bitcoin, huku wakiwataka wafuasi wa akaunti hiyo kutuma pesa kupitia Bitcoin na baadae warudishiwe mara mbili ya pesa walizotuma kupitia Bitcoin. Unaweza kuona baadhi ya Tweets hizo kupitia hapo chini.

Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa

Kwa sasa bado Twitter inaendelea na uchunguzi ili kujua udukuzi huu umefanyika na nani au kikundi gani cha watu. Kwa taarifa zaidi endelea kutembelea Tanzania Tech.

Akaunti za Twitter za Kampuni Kubwa na Watu Maarufu Zadukuliwa
Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Elon Musk Azindua Mfumo wa Akili Bandia (AI) xAI Grok

Written by Amani Joseph

Tanzania Tech tumejikita kuhakikisha hupitwi na habari yoyote ya teknolojia, endelea kuwa nasi tufuate kwenye mitandao ya kijamii.

Toa Maoni Hapa

Kumbuka ni Muhimu Kuandika Jina Halisi na Barua Pepe, Vigezo na Masharti Kuzingatiwa.