Huawei Mbioni Kuzindua Simu Mpya ya Huawei Mate 20

Zifahamu hizi hapa sifa za awali za Simu mpya ya Huawei Mate 20
Simu mpya ya Huawei Mate 20 Simu mpya ya Huawei Mate 20

Kampuni ya Huawei iko mbioni kuja na simu yake mpya ya Huawei Mate 20, Kama ilivyokuwa kwenye simu za Huawei P20 na P20 Pro, simu hiyo mpya ya Huawei Mate 20 nayopia inatarajiwa kuangalia zaidi kwenye upande wa kamera pamoja na mfumo wa AI.

Kwa mujibu wa tovuti ya GSMArena simu hiyo mpya ya huawei Mate 20 inatarajiwa kuja na kamera tatu kwa nyuma huku zikiwa kwenye mtindo mpya tofauti na ambavyo watu wamezoea au jinsi simu nyingi zinavyokuwa.

Mbali na hayo simu hii mpya ya Huawei Mate 20 inatarajiwa kuja na mfumo wa Android 9 Pie, Processor kutoka kwa Huawei ya HiSilicon Kirin 980 inayo saidiwa na RAM ya GB 6 pamoja na ukubwa wa ndani wa GB 128. Kioo cha Huawei Mate 20 kinakuja na ukubwa wa inch 6.3 kilicho tengenezwa kwa teknolojia ya AMOLED, ambacho pia kinakuja na resolution ya 2244×1080.

Advertisement

Simu hii inatarajiwa kuja kwa matoleo matatu ikiwa pamoja na Huawei Mate 20, Mate 20 Pro na Huawei Mate 20 Porsche Edition ambazo zote zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi ujao tarehe 16 october 2018.

Kwa sasa ili kujua zaidi kuhusu simu hii endelea kutembelea Tanzania Tech tutakuletea uzinduzi wa simu hii mubashara kabisa kupitia hapa hapa.

2 comments

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use