Mozilla Yaleta Njia Mpya ya Kutuma na Kupokea Mafaili

Sasa tumia mozilla kutuma na kupokea mafaili kwa urahisi masaa 24
mozilla mozilla

Kuna wakati unataka kutuma faili la aina flani hivyo inakubidi kutumia njia mbalimbali kama vile email, whatsApp pamoja na programu nyingine kama hizo lakini kampuni ya mozilla ina-kuleta njia mpya ya kutuma na kupokea ma-faili ya aina mbalimbali kwa urahisi kabisa.

Sehemu hiyo ambayo ipo kwenye majaribio inakupa uwezo wa kutuma ma-faili yenye ukubwa wa hadi GB 1 tu, utofauti wa sehemu hiyo ni kuwa utapewa nafasi ya kutuma ma-faili ambayo baadae yata futika ndani ya masaa 24, hivyo kila link inauwezo wa kudumu masaa 24 pekee.

Advertisement

Kuwezesha sehemu hiyo huna haja ya kuwa na kisakuzi cha Mozilla bali unachotakiwa kufanya ni kubofya link hapo chini kisha upload file lako kisha mtumie link mtu unaetaka apate file hilo kisha ataweza kudownload file hilo haraka kabisa bila kupoteza muda.

send.firefox.com

Njia hii ambayo imetengenezwa na kampuni ya mozilla ina semekana kuwa ni njia ambayo ni salama sana na mafaili yote yanayo tumwa kupitia sehemu hii yana kuwa encrypted hivyo huna haja ya kuwa na wasiwasi pale unapo taka kuitumia.

Kwa habari zaidi za teknolojia endelea kutembelea Tanzania Tech pia unaweza kudownload App ya Tanzania Tech ili kupata habari zote za teknolojia kwa haraka, pia usisahu kujiunga na channel yetu ya Tanzania Tech ili kupata habari na maujanja mbalimbali ya teknolojia kwa njia ya Video.

Chanzo : Tech Crunch

Add a comment

Toa Jibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Pata Habari za Teknolojia Kupita Barua Pepe

By pressing the Subscribe button, you confirm that you have read and are agreeing to our Privacy Policy and Terms of Use